Ujana nini? Na Kijana ni nani?

Ujana ni hatua ambayo mtu anafikia na kuanza kupevuka kiakili na kutokufikiria vile ambavyo alikuwa anafikiria kipindi akiwa na umri wa kitoto hapa unatakiwa aanzae kujitegema katika kufikri na kuweza hata kuwasaidia wengine.

Kijana ni suala la mtu kujinasibu kwa ujana ni suala la umri pekee. Kwamba mimi nina miaka 25 basi miaka hii ni kigezo tosha cha kuwa kijana.Naweza kukuambia ya kwamba ujana sio umri tu bali ni zaidi ya umri. Mimi nimekuwa nikijiuliza je, kwa mazingira yetu(tz) vijana ni akina nani? Je, ni wale wanaojitahidi kufikiri kwa mantiki na kutoa majawabu kwa baadhi ya matatizo yanayozunguka jamii au ni wale waliogeuka vidaka tonge kwa kukubali kutumiwa na waovu wenye uchu na mali iwe katika siasa, madhehebu ya dini, n.k.Je, ujana ni kuwa na msimamo wenye kuogozwa na hoja zenye mashiko na uthubutu katika kuchochea maendeleo ya jamii au ni kujisalimisha kwa waovu na kuwatetea kwa nguvu zote katika harakati zao (kisiasa,kiuchumi n.k) na kutegemea kuambulia makombo. Je, vijana tunafikiri au haki yetu ya kufikiri tumeirasimisha kwa wengine (wenye uwezo na umaarufu). NAOMBA TUTAFAKARI PAMOJA.

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Twitter picture

You are commenting using your Twitter account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s